Monday, March 31, 2014
Friday, March 28, 2014
Eti Mungu wa Biblia ni Kahaba Kulingana na Isaya 23:17-18
Kama kawaida yao, Waislamu wanaendelea
kudanganywa na walimu wao na kujipa matumaini kuwa wako kwenye njia ya uzima
kutokana na kile wanachoamini kuwa Biblia si Neno la Mungu bali Quran ndiyo
Neno la Mungu.
Kwa sababu wanaonekana ni watu wasiokuwa na
utayari wa kuchunguza kile wanachoambiwa, basi wanaamini kila uongo na udanganyifu wanaopewa na kuubeba kama ulivyo na kuutangaza kwa ujasiri kabisa kana kwamba ndiyo kweli halisi!
Thursday, March 27, 2014
Unabii wa Kifo cha Yesu Kupitia Ibrahimu na Isaka
Kuzaliwa na kufa kwa Bwana
Yesu si jambo lililoibuka tu. Hili lilikuwa ni jambo ambalo tangu wakati wa
kosa la Adamu na Hawa katika bustani ya Edeni lilitolewa unabii na Mungu
mwenyewe. Mungu alimwambia shetani:“nami nitaweka uadui kati yako na huyo
mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na
wewe utamponda kisigino.” (mwanzo 3:15).
Hakuna mwanadamu anayeitwa
uzao wa mwanamke. Uzao huwa unahesabiwa kwa manamume siku zote na duniani kote.
Lakini ni Yesu peke yake ambaye hakuzaliwa na baba wa kibinadamu kama wanadamu
wengine ndiyo maana anaitwa uzao wa mwanamke.
Wakati wa Ibrahimu, Mungu
alitoa tena unabii juu ya kufa, kufufuka na kulipa dhambi kwa Bwana Yesu.
Unabii huu ulitolewa kupitia mtoto wa Ibrahimu, yaani Isaka. Je, ilikuwaje?
Tuesday, January 14, 2014
Eti Yesu Amelaaniwa Hawezi Kuokoa
Kwenye
facebook kuna hoja nyingi zinazozungumziwa humo. Nikakutana na ndugu mmoja mwislamu anatoa
hoja kwamba Yesu amelaaniwa, hivyo hana uwezo wa kuokoa mtu. Na anatoa kabisa
maandiko ya Biblia, eti kuthibitisha hoja zake - si kwa kudhihaki, bali kwa kuamini kabisa kwamba hivyo ndivyo ilivyo! Na hivi ndivyo hali ilivyo
kabisa kwa Waislamu linapokuja suala la kutafuta sababu za wao kuukataa wokovu
wa Yesu Kristo.
Monday, January 6, 2014
Maswali yangu kwako Mwislamu
Tarehe 21 Desemba 2012 niliuliza
maswali yafuatayo HAPA. Lakini umepita mwaka mzima bado sijapata jibu japo kwa
swali hata mojawapo tu! Ina maana maswali haya hayana majibu kutoka kwenye
Quran au labda ndugu zangu Waislamu hawajayaona? Of course mimi binafsi najua
kuwa hawawezi kuyajibu kwa sababu Uislamu hauna majibu juu ya masuala ya
rohoni.
Hata hivyo, ningependa niyaulize kwa mara nyingine tena
hapa tunapoanza mwaka huu wa 2014 ili iwe changamoto kwa Mwislamu uwaye yote –
ujihoji, ujiulize na ujipime kule uendako.
Friday, November 15, 2013
Urithi wa Uislamu kutoka kwenye dini za kipagani za Uarabuni – Sehemu ya 2
Ka’aba
Katika sehemu ya 1 ya makala haya tuliangalia kuhusu asili ya Allah. Katika sehemu hii ya 2 tutaongelea kuhusiana na mji wa Makka na ka'aba, ambayo ni madhabahu kuu ya Uislamu.
Mji wa Makka ndio kitovu cha Uislamu duniani. Kwenye mji huu ndiko iliko Ka’aba, au kama wanavyoamini na kuiita Waislamu Bait – ul- Haram; au Bait – ul- Allah, yaani ‘nyumba ya Allah’ au ‘nyumba ya Mungu’. Na kila Mwislamu kokote duniani anatakiwa kuswali swala 5 kila siku huku akielekeza uso wake Makka iliko hiyo nyumba ya Mungu wao. Vilevile, kila mmoja wao anatakiwa kwenda Makka kuhiji walau mara moja katika maisha yake, maana hija ni moja ya nguzo kuu katika Uislamu. Kwa maana nyingine, Ka’aba ndiyo madhabahu kuu katika Uislamu.
Mji wa Makka ndio kitovu cha Uislamu duniani. Kwenye mji huu ndiko iliko Ka’aba, au kama wanavyoamini na kuiita Waislamu Bait – ul- Haram; au Bait – ul- Allah, yaani ‘nyumba ya Allah’ au ‘nyumba ya Mungu’. Na kila Mwislamu kokote duniani anatakiwa kuswali swala 5 kila siku huku akielekeza uso wake Makka iliko hiyo nyumba ya Mungu wao. Vilevile, kila mmoja wao anatakiwa kwenda Makka kuhiji walau mara moja katika maisha yake, maana hija ni moja ya nguzo kuu katika Uislamu. Kwa maana nyingine, Ka’aba ndiyo madhabahu kuu katika Uislamu.
Monday, November 11, 2013
Urithi wa Uislamu kutoka kwenye dini za kipagani za Uarabuni - sehemu ya 1
Allah
alitokea wapi?
Uislamu unajinadi kwamba
Allah ndiye Mungu yuleyule aliyejishughulisha ya Wayahudi tokea nyakati za Ibrahimu
katika Agano la Kale. Je, jambo hilo ni kweli?
Uislamu ulianza na
Muhammad kwenye miaka 600 baada Kristo. Je, kabla yake imani za Waarabu
zilikuwaje? Je, yako mambo yoyote kutoka kwenye imani hizo ambayo yaliingia
kwenye Uislamu? Kwa maneno mengine, je, Uislamu hauna upagani ndani yake?
Fuatana nami kwenye makala
haya marefu yanayochambua chimbuko la Uislamu ili tuweze kuona iwapo upo uhusiano
wowote kati ya Uislamu na upagani uliokuwa ukitawala miongoni mwa jamii za Waarabu
kabla ya kutokea kwa Muhammad?
Sunday, August 25, 2013
Mungu Amwonyesha Nabeel Njia ya Kweli Kati ya Uislamu na Ukristo - Sehemu ya 2
Katika sehemu ya kwanza ya
ushuhuda huu wa Nabeel, aliyekuwa Mwislamu kisha akakutana na Bwana Yesu na
kupokea wokovu, tuliona jinsi ambavyo alimwomba Mungu ampe maono
yatakayomwonyesha imani ya kweli. Alionyeshwa misalaba kwenye maono lakini yeye
akasema labda ni macho yake tu yamemchezea mchezo. Kwa hiyo, alimwomba tena
Mungu kwamba, kama yale maono yalitoka kwake, basi ayathibitishe kwa ndoto. Je,
Mungu alifanya nini? Tafadhali endelea kusoma sehemu hii ya pili.
Saturday, August 24, 2013
Mungu Amwonyesha Nabeel Njia ya Kweli Kati ya Uislamu na Ukristo - Sehemu ya 1
Nabeel alizaliwa na
kukulia kwenye familia na maisha ya kiislamu. Uislamu ulikuwa ni kila kitu
kwake. Lakini wakati ulipofika wa yeye kujua jema na baya, alianza kujihoji
kuhusu maisha yake, Mungu wake, na hatima yake ya milele. Hatimaye alimwomba
Mungu amwonyeshe kweli. Je, nini kilitokea? Tafadhali fuatilia sehemu hii ya
kwanza ya ushuhuda huu.
Friday, July 26, 2013
Yesu Aongea na Binti wa Kiislamu; Binti Aokoka
Sharoni hakuwa Mkristo
bali alikuwa ni binti wa Kiislamu. Na wala hakuwa amewahi kujifunza habari za
Yesu na Ukristo. Lakini Bwana Yesu mwenyewe alimfuata na kujidhihirisha kwake. Je,
ilikuwaje, na nini kilitokea baada ya hapo? Tafadhali fuatilia ushuhuda huu
wenye nguvu na unaodhihirisha upendo na uweza na uungu wa Bwana Yesu.
Sunday, July 14, 2013
Toufik Alikuwa Mwislamu Lakini Alimwita Yesu, Leo Ameokolewa na Hajawahi Kujuta
Ufuatao ni ushuhuda wa Toufik, ambaye alikuwa ni Mwislamu lakini alikutana na injili ya Bwana Yesu na kubadili welekeo ambao hajaujutia; na hata anapoelezea neema hii ya wokovu wa Yesu aliyoipata, machozi yanamtoka. Pia machozi yanamtoka zaidi anapowafikiria ndugu zake Waislamu ambao wanapambana kwa jitihada nyingi wakijaribu kumpendeza Mungu kwa njia ya matendo yao ya kidini. Toufik analia anapotambua kuwa yote hiyo wanayofanya ni kazi bure kwa kuwa hawajagundua ziri ambayo na yeye, miaka mingi iliyopita, alikuwa hakuijua.
Thursday, July 11, 2013
Kufa kwa Yesu Kristo Maana Yake Nini?
Utakatifu
Mungu ni
mtakatifu. Kutenda dhambi ni kukosa utii kwa Mungu. Mungu anasema kwenye Neno
lake: Basi mtakuwa watakatifu, kwa kuwa mimi ni
Mtakatifu. (Walawi 11:45).
Pia imeandikwa: Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi
iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa
watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu (1 Petro
1:15).
Kwa
kifupi, kuwa mtakatifu maana yake ni kutokuwa na dhambi yoyote. Mungu kamwe
hawezi kufumbia macho dhambi hata iwe ni moja. Kamwe! Hafumbii macho hata zile
dhambi ambazo sisi tunaziona ni ndogo sana.
Saturday, July 6, 2013
Je, ni Kweli Quran Haijawahi Kubadilika na Wala Haina Mkono wa Mwanadamu Ndani Yake?
Utangulizi
Rafiki yangu Ibra, amekuwa akinishambulia sana kwa kusema
kuwa Biblia ni kitabu kisichoaminika bali Quran ndiyo inayopaswa kuaminiwa.
Hoja yake kuu, kama ilivyo kwa Waislamu wengine wengi ni kwamba, Biblia
imeingizwa maneno ya kibinadamu kiasi kwamba yale ambayo Mungu aliyateremsha ni
kama hayapo tena leo.
Katika makala haya ninapenda tuangalie swali kwamba:
Je, ni kweli Quran ni kitabu ambacho hakijawahi kubadilika? Je, ujumbe wake
ndio uleule ambao aliteremshiwa Muhammad na Allah? Je, ni kitabu cha kuaminika
kuliko Biblia kama wanavyosema Waislamu?
Friday, July 5, 2013
Je, Biblia Ina Vitabu Vingapi?
Vitabu 73 au 66?
Leo duniani
kuna Biblia yenye vitabu 73 na yenye vitabu 66. Waislamu wamekuwa wakitumia
suala hili kama silaha ya kushambulia Biblia kwamba ni kitabu kisichoaminika,
wala hakiwezi kumfikisha mtu mbinguni.
Kwa mfano,
ndugu yangu Ibra ambaye amekuwa msomaji na mchangiaji mzuri sana wa blog hii
ameniuliza kama ifuatavyo:
James,
naomba majibu kwa maswali yafuatayo:
-Biblia original kabisa iliyoandikwa na roho mtakatifu ina vitabuvingapi?
-Kitabu cha Danieli kina sura 12 au 14?
-Biblia yenye vitabu 73 na ile ya 66 ipi ya kweli? Je! Hapa kuna mkono wa roho mtakatifu au ubinadamu?
Ukweli unabaki palepale kwamba biblia sio kitabu cha kutegemea sana kwa mambo ya mungu. Hapa duniani biblia ninazojua mimi ziko zaidi ya tano. Na zote zimepishana kwa namba ya vitabu vilivyopo.
Sasa hapo mimi nabaki nashangaa, niamini biblia gani kati ya hizi? Ubabaishaji, kweli haimo.
Tafakari. Jihoji. Kweli imo ndani yako! Soma Qur'ani tukufu.
-Biblia original kabisa iliyoandikwa na roho mtakatifu ina vitabuvingapi?
-Kitabu cha Danieli kina sura 12 au 14?
-Biblia yenye vitabu 73 na ile ya 66 ipi ya kweli? Je! Hapa kuna mkono wa roho mtakatifu au ubinadamu?
Ukweli unabaki palepale kwamba biblia sio kitabu cha kutegemea sana kwa mambo ya mungu. Hapa duniani biblia ninazojua mimi ziko zaidi ya tano. Na zote zimepishana kwa namba ya vitabu vilivyopo.
Sasa hapo mimi nabaki nashangaa, niamini biblia gani kati ya hizi? Ubabaishaji, kweli haimo.
Tafakari. Jihoji. Kweli imo ndani yako! Soma Qur'ani tukufu.
Wednesday, June 26, 2013
Swali kwa Waislamu Kuhusu Kupotoshwa kwa Biblia
Je, Biblia ni Kitabu Kilichopotoshwa na Wanadamu?
Waislamu wanashikilia SANA kwamba Biblia imepotoshwa;
na kwamba Quran ndicho kitabu cha kweli chenye ujumbe wa kweli wa Mungu aliye
hai.
Baada ya Yesu kuondoka Duniani, Quran ilikuja miaka
zaidi ya 600 baadaye. Biblia ilishakuwapo kwa maelfu ya miaka kabla ya hapo.
Baada ya Quran kuandikwa, ikasema mengi kuhusiana na
Biblia, yakiwamo machache yafuatayo:
Subscribe to:
Posts (Atom)










