Showing posts with label yeremia 8:8. Show all posts
Showing posts with label yeremia 8:8. Show all posts

Sunday, March 17, 2013

Majibu Yangu kwa Ibrabura - Sehemu ya 2



JE, BIBLIA NI KITABU KILICHOPOTOSHWA?

Yeremia 8:8 inasema kwamba: Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.


Waislamu walipoona maneno haya: “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo,” kama kawaida, wakajua kuwa huu tayari ni ushahidi kwamba Biblia imetiwa maneno ya uongo, kwa hiyo si Neno la Mungu na haiwezi kuaminika.


Lakini mara zote ni lazima kwenda kwenye muktadha wa kila andiko au hoja ili kuona kama kweli hoja hizo zina nguvu ya kusimama.