JE, BIBLIA NI KITABU KILICHOPOTOSHWA?
Yeremia
8:8 inasema kwamba: Mwasemaje, Sisi tuna akili, na
torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya
waandishi imeifanya kuwa uongo.
Waislamu
walipoona maneno haya: “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo
pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa
uongo,” kama kawaida, wakajua kuwa huu tayari ni ushahidi kwamba Biblia imetiwa
maneno ya uongo, kwa hiyo si Neno la Mungu na haiwezi kuaminika.
Lakini
mara zote ni lazima kwenda kwenye muktadha wa kila andiko au hoja ili kuona
kama kweli hoja hizo zina nguvu ya kusimama.
