Tuesday, January 14, 2014

Eti Yesu Amelaaniwa Hawezi Kuokoa




Kwenye facebook kuna hoja nyingi zinazozungumziwa humo. Nikakutana na ndugu mmoja mwislamu anatoa hoja kwamba Yesu amelaaniwa, hivyo hana uwezo wa kuokoa mtu. Na anatoa kabisa maandiko ya Biblia, eti kuthibitisha hoja zake - si kwa kudhihaki, bali kwa kuamini kabisa kwamba hivyo ndivyo ilivyo! Na hivi ndivyo hali ilivyo kabisa kwa Waislamu linapokuja suala la kutafuta sababu za wao kuukataa wokovu wa Yesu Kristo.