Tuesday, January 15, 2013

Hata Saudi Arabia Bwana Yesu Ameingia


Mhalifu wa kidini akihukumiwa kwa mujibu wa sharia
[Kama unachofanya ni kizuri; ni cha Mungu, kwa nini ufiche uso?]

Waislamu Wanazidi kukutana na Yesu

na Grantley Morris
‘. . . shuhuda zaidi na zaidi zinakuja kutoka kwenye nchi zilizofungwa juu ya Mungu anavyowapa Injili Waislamu kwa namna isiyo ya kawaida kupitia ndoto na maono. Miongoni mwa maelfu ya waamini katika Irani katika miaka michache iliyoisha, zaidi ya nusu yao wamekuwa waamini baada ya Yesu mwenyewe kuwatokea katika ndoto au maono.’ Wendell Evans wa the Billy Graham Center’s Institute for Muslim Studies anazungumzia juu ya wingi wa ndoto na maono yanayoripotiwa kuhusu Kristo miongoni mwa Waislamu . . .’

Kuzimu

Abdullah alikuwa Mwislamu mwaminifu. Aliishi umbali wa kama saa moja hivi kwa mwendo wa gari kutoka Makka. Alikuwa akiswali mara tano kwa siku, na mara kwa mara alitembelea Makka.

Kama ilivyo kwa Waislamu wengi, Abdullah alifundishwa kuwa Wakristo wana pepo wachafu na kwamba anatakiwa kujiepusha nao.

Usiku mmoja Abdullah aliota ndoto kwamba yuko kuzimu, anaungua moto. Asubuhi iliyofuata, akiwa ana wasiwasi mkubwa, aliomba kwa Allah, ‘Nimefanya kila kitu vizuri; kwa nini niende motoni?’ katika ziku zilizofuata, aliendelea kupata wasiwasi zaidi.