Thursday, March 27, 2014

Unabii wa Kifo cha Yesu Kupitia Ibrahimu na Isaka




Kuzaliwa na kufa kwa Bwana Yesu si jambo lililoibuka tu. Hili lilikuwa ni jambo ambalo tangu wakati wa kosa la Adamu na Hawa katika bustani ya Edeni lilitolewa unabii na Mungu mwenyewe. Mungu alimwambia shetani:“nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.” (mwanzo 3:15).

Hakuna mwanadamu anayeitwa uzao wa mwanamke. Uzao huwa unahesabiwa kwa manamume siku zote na duniani kote. Lakini ni Yesu peke yake ambaye hakuzaliwa na baba wa kibinadamu kama wanadamu wengine ndiyo maana anaitwa uzao wa mwanamke.

Wakati wa  Ibrahimu, Mungu alitoa tena unabii juu ya kufa, kufufuka na kulipa dhambi kwa Bwana Yesu. Unabii huu ulitolewa kupitia mtoto wa Ibrahimu, yaani Isaka. Je, ilikuwaje?