Tuesday, March 27, 2018

Ukipenda kuona utaona - ni uamuzi wako tu


Ibilisi akitupwa chini pamoja na majini yake

Kwenye Biblia katika kitabu cha Isaiah 14:12 tunasoma:

Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!

Aya hii inamwongelea Lusifa (ibilisi/shetani) jinsi ambavyo zamani alikuwa juu lakini akaangushwa chini kwa sababu ya uovu wake.

Kwenye aya hii, ibilisi anaitwa “nyota ya alfajiri”.
Kwa Kiebrania, jina hili ni heylel ben shachar.

Waarabu, wao wana neno hilal, ambalo maana yake ni “mwezi mchanga.”
Na hata Kiswahili nacho kimechukua neno hilo – “hilali”

Kwa hiyo, tunaweza kusema kuwa huyu “nyota ya alfajiri” anaweza pia kuitwa “mwezi mchanga (mwandamo) mwana wa alfajiri.”

Kwa mujibu wa Isaya 14:12 tuliyoanza nayo hapo juu, tumeona kuwa aya hiyo inamwongelea ibilisi. Kwa hiyo, huyu “mwezi mchanga (mwandamo) mwana wa alfajiri” ni Lusifa au ibilisi mwenyewe.

Ukisogea mbele kidogo na kusoma Isaya 14:13-14, Isaya anaendelea kumwongelea huyu ibilisi kwa namna hii:

Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.

Huyu ibilisi anataja mambo makubwa mawili:
Moja: Nitapanda mpaka mbinguni.
Mbili: Nitafanana nay eye aliye juu.

Kwa hiyo, tangu zamani ibilisi alitamani kuwa juu ya nyota za mbinguni (nyota hapa ni malaika). Na lengo lake ni ili afanane na Muumba wake; aogopwe kama Mungu; aabudiwe kama Mungu.

Na hicho ndicho kilichosababisha akatupwa nje ya mbingu hadi huku chini.

Ndio maana tunasoma kwenye kitabu cha Ufunuo 12:7-9

Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

Lakini je, nia yake ya kuabudiwa kama Mungu aliiacha?

Ukienda kwenye Biblia ya lugha yake ya asili (Kiebrania), neno kupanda ni alah.
Ili kuthibitisha hilo, google: “Strongs Hebrew Greek Dictionary H5927”





Sasa hebu jiulize:

Hili jina liko hapa kwa bahati mbaya?
Je, kwa nini mwezi na nyota huinuliwa juu kwenye misikiti?



Mat 11:25
Wakati ule yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga.

Ndugu yangu, chagua uzima sasa kabla mlango haujafungwa:
 
Yoh 14:6
Yesu akamwambia, mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

No comments:

Post a Comment