Sunday, January 13, 2013

Jambo la Ajabu Linaendelea Kwenye Ulimwengu wa Kiislamu




Makala haya yanaelezea mahojiano yaliyofanywa na mtangazaji wa CBN, Chris Mitchel, kuhusiana na kile kinachoendelea katika ulimwengu wa Kiislamu, ambao kwa karne nyingi umekuwa ukipinga kabisa Injili kuhubiriwa kwenye sehemu hiyo. Mahojiano haya yanaonyesha jinsi ambavyo Bwana Yesu mwenyewe anabomoa kuta na vizuizi kwa namna ambayo hata tawala za kiimla zinazotumia mahakama, hukumu za kifo na sheria kali kuzuia Injili kuwafikia watu, hawana tena la kufanya. Ni wakati wa Waislamu kujihoji na kumpokea Mwokozi wao ambaye aliwafia msalabani.

Mwanamke Mwislamu Aliyemkimbilia Yesu Kristo


Hii si picha ya Siti mwenyewe. Ni picha tu kutoka kwenye mtandao.

Ushuhuda wa Siti Zainab

Assalam-mualaikum.

Jina langu ni Siti Zainab. Mimi ni mwanamke wa Kiislamu kutoka Malesia, kusini mashariki mwa Asia.  Nilizaliwa kwenye familia ya Kiislamu, iliyokuwa ikifuata taratibu za Kiislamu kwa nguvu sana. Tokea mwanzo, nilipata elimu ya Kiislamu ambayo ilikuwa imara na ya ndani sana.

Pamoja na elimu yangu ya msingi, nilipelekwa pia kwenye madrasah ya Kiislamu, yaani shule ya dini, na nikaanza kusoma na kukariri Quran tangu mapema; huku nikijifunza maadili na misingi ya Uislamu wa Kisuni, kutoka kwa walimu waliobobea wa Kiislamu. Huko nilijifunza kumwogopa na kumtii Allah s.w.t. na pia kufuata mafundisho na mifano ya Mtume Muhammad (hususani yale yaliyo kwenye Hadithi zinazokubalika). Pia nilikuwa nina uwezo wa kusoma Quran yote, jambo ambalo liliwafurahisha wazazi wangu. Kwa kifupi, nilikuwa nina msingi imara na imani ya ndani ya dini kama Muslimah mwaminifu na aliyejitoa kwa moyo wote.