Thursday, July 11, 2013

Kufa kwa Yesu Kristo Maana Yake Nini?




Utakatifu

Mungu ni mtakatifu. Kutenda dhambi ni kukosa utii kwa Mungu. Mungu anasema kwenye Neno lake: Basi mtakuwa watakatifu, kwa kuwa mimi ni Mtakatifu. (Walawi 11:45).

Pia imeandikwa: Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu (1 Petro 1:15).

Kwa kifupi, kuwa mtakatifu maana yake ni kutokuwa na dhambi yoyote. Mungu kamwe hawezi kufumbia macho dhambi hata iwe ni moja. Kamwe! Hafumbii macho hata zile dhambi ambazo sisi tunaziona ni ndogo sana.