Saturday, February 23, 2013

Bwana Yesu Asema na Miryam wa Saudia Kupitia Ndotoni





Ufuatao ni ushuhuda wa dada aitwaye Miryam, kutoka Saudi Arabia, ambaye Bwana Yesu alisema naye kupitia ndotoni. Matokeo yake, dada Miryam alitoka kwenye Uislamu na sasa anamwamini Yesu kama Bwana na Mwokozi wake.


Katika video ya hapo juu, Miryam anahojiwa na mwendeshaji wa kipindi kiitwacho “God of Mracles” au “Mungu wa Miujiza” kinachorushwa na kituo cha TV cha “Jesus Set Me Free”, au “Yesu aliniweka Huru.”


Fuatana na mtangazaji katika mahojiano haya yenye kuonyesha jinsi Bwana Yesu mwenyewe anavyofanya kazi kwenye nchi za Kiarabu ambazo, wao wanadhani kuwa sheria kali zitazuia Injili ya Bwana kupenya. Hawajui kuwa kuta na ngome walizowafungia watu na kuwanyima uhuru zinabomokabomoka na anayezibomoa ni Bwana mwenyewe kwa namna ambao hawana kamwe nguvu ya kuizuia.