Sunday, February 3, 2013

Muhubiri wa Kiislamu Kutoka Misri Aokoka Baada ya Yesu Kusema Naye Kupitia Ndotoni



Ibrahim alikuwa Mwislamu wa imani kali. Alikuwa mtoa mihadhara katika misikiti mbalimbali nchini Misri. Alikutana na Injili ya Yesu. Moyo wake ulitikiswa. Hakujua amwamini nani – je, ni Yesu au ni Muhammad? Nani angemwambia njia ya kweli ni ipi? Aliinua moyo wake juu mbinguni. “Yehova, nionyeshe njia ya kweli nami nitaifuata kwa gharama yoyote ile,” alisema kwa machozi.

Bwana Yesu mwenyewe alikuja kusema na Ibrahim katika ndoto. Ibrahim aliachana na Uislamu na kumkumbatia Mwokozi. Lakini kundi la Waislamu wenye imani kali la Muslim Brotherhood wangemwacha tu? Vipi kuhusu familia yake?

Kumfuata Kristo kuna gharama. Lakini huwezi kumbadilisha mtu anapomjua Mungu wa kweli ingawaje utampiga, utamfunga, na kumtesa kwa kila namna. Endelea kusoma ushuhuda huu wa kutia moyo na Mungu wa mbinguni atasema na moyo wako kwa njia ya ajabu ambayo itabadilisha kabisa maisha yako....!