Tuesday, February 19, 2013

Maisha ya Wanawake Katika Nchi za Kiislamu





Mwanamke wa Saudia aliyeamua kuumwaga
moyo wake wote


Ni jambo lililo wazi kwamba wanawake katika nchi za Kiislamu wananyanyaswa kupita kiasi. Maisha yao hayana uhuru wala amani kwa kuwa sheria za dini yao zinawakandamiza wao na kuwapendelea wanaume. Hata hivyo, baadhi yao wanatambua hali hiyo na wanapambana kujaribu kuibadilisha. Lakini, ni wazi pia kuwa mapambano yao hayo hayawezi kuwasaidia sana kwa kuwa huko ni sawa na kusema Quran ibadilishwe. Je, hilo linawezekana kwa nchi hizo? Maana tatizo si wanaume au serikali; tatizo ni maagizo ya Mungu wanayemwabudu.


Katika video hiyo hapo juu, tunamwona mwanamke mtangazaji wa kituo kimojawapo cha TV kule Saudi Arabia, akimhoji mwanamke mwingine, Bi. Buthayna Nasser, ambaye naye ni mtangazaji kwenye kituo cha TV. Mahojiano yanahusu mjadala uliokuwamo kati ya wanazuoni wa Saudia juu ya wanawake kuonyesha nyuso zao kwenye TV ya Saudia.