Thursday, November 2, 2017

Ujumbe wa Muhammad haukutoka kwa Mungu wa kweli


 

Muhammad si tu kwamba ni mtume ambaye hashuhudiwi na binadamu mwingine yeyote bali pia namna alivyokuwa akipata ufunuo (wahyi) wake ni jambo linalotia mashaka makubwa sana.

Hashuhudiwi na binadamu mwingine yeyote kwa sababu mambo yote aliyosema yanatoka kinywani mwake peke yake na hakuna mtu wa pili wa kusimama kama shahidi ili kuonyesha kuwa alichosema ni kweli kinatoka kwa Mungu wa mbinguni.

Yaani shahidi wa mambo yake ni yeye peke yake.
Na hakimu wa mambo yake ni yeye peke yake.