Monday, March 31, 2014

"Sikuja kutangua torati" maana yake ni nini?




Bwana Yesu alisema: Msidhani ya kuwa nalikuja kutangua torati au manabii, la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie.(Mt. 5:17-18). Ni nini maana ya andiko hili?

Friday, March 28, 2014

Eti Mungu wa Biblia ni Kahaba Kulingana na Isaya 23:17-18




Kama kawaida yao, Waislamu wanaendelea kudanganywa na walimu wao na kujipa matumaini kuwa wako kwenye njia ya uzima kutokana na kile wanachoamini kuwa Biblia si Neno la Mungu bali Quran ndiyo Neno la Mungu.

Kwa sababu wanaonekana ni watu wasiokuwa na utayari wa kuchunguza kile wanachoambiwa, basi wanaamini kila uongo na udanganyifu wanaopewa na kuubeba kama ulivyo na kuutangaza kwa ujasiri kabisa kana kwamba ndiyo kweli halisi!

Thursday, March 27, 2014

Unabii wa Kifo cha Yesu Kupitia Ibrahimu na Isaka




Kuzaliwa na kufa kwa Bwana Yesu si jambo lililoibuka tu. Hili lilikuwa ni jambo ambalo tangu wakati wa kosa la Adamu na Hawa katika bustani ya Edeni lilitolewa unabii na Mungu mwenyewe. Mungu alimwambia shetani:“nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.” (mwanzo 3:15).

Hakuna mwanadamu anayeitwa uzao wa mwanamke. Uzao huwa unahesabiwa kwa manamume siku zote na duniani kote. Lakini ni Yesu peke yake ambaye hakuzaliwa na baba wa kibinadamu kama wanadamu wengine ndiyo maana anaitwa uzao wa mwanamke.

Wakati wa  Ibrahimu, Mungu alitoa tena unabii juu ya kufa, kufufuka na kulipa dhambi kwa Bwana Yesu. Unabii huu ulitolewa kupitia mtoto wa Ibrahimu, yaani Isaka. Je, ilikuwaje?