Friday, April 18, 2014

Eti Wakristo Hula Mkate Wenye Mavi (au Mashonde)





Waislamu wanaojaribu kuitoa makosa Biblia bado wanaendelea na mahangaiko yao ya kujaribu kuipa uhalali quran kupitia upotoshaji mkubwa wa Maandiko ya Biblia. Kama kwaida, hawana hoja mpya wala za kufikirisha, bali ‘wana-recycle’ maswali yaleyale toka januari hadi desemba. Haya ni maswali ambayo yalibuniwa na watu fulanifulani, basi na wao wanayabeba bila hata ya kuchuja na kujua endapo yana ukweli au la. Hata hivyo, kila jambo wanalolisema kinyume na Biblia ni UONGO mtupu SIKU ZOTE - NA USHAHIDI WA UONGO HUO TUNAO WAZIWAZI!

Katika kitabu cha Ezakieli imeandikwa:

…. Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya mashonde yatokayo katika mwanadamu. (Eze 4:12).
[Maana ya mashonde ni kinyesi]