Showing posts with label mwanamke wa kiislamu. Show all posts
Showing posts with label mwanamke wa kiislamu. Show all posts

Saturday, February 23, 2013

Bwana Yesu Asema na Miryam wa Saudia Kupitia Ndotoni





Ufuatao ni ushuhuda wa dada aitwaye Miryam, kutoka Saudi Arabia, ambaye Bwana Yesu alisema naye kupitia ndotoni. Matokeo yake, dada Miryam alitoka kwenye Uislamu na sasa anamwamini Yesu kama Bwana na Mwokozi wake.


Katika video ya hapo juu, Miryam anahojiwa na mwendeshaji wa kipindi kiitwacho “God of Mracles” au “Mungu wa Miujiza” kinachorushwa na kituo cha TV cha “Jesus Set Me Free”, au “Yesu aliniweka Huru.”


Fuatana na mtangazaji katika mahojiano haya yenye kuonyesha jinsi Bwana Yesu mwenyewe anavyofanya kazi kwenye nchi za Kiarabu ambazo, wao wanadhani kuwa sheria kali zitazuia Injili ya Bwana kupenya. Hawajui kuwa kuta na ngome walizowafungia watu na kuwanyima uhuru zinabomokabomoka na anayezibomoa ni Bwana mwenyewe kwa namna ambao hawana kamwe nguvu ya kuizuia.

Tuesday, February 19, 2013

Maisha ya Wanawake Katika Nchi za Kiislamu





Mwanamke wa Saudia aliyeamua kuumwaga
moyo wake wote


Ni jambo lililo wazi kwamba wanawake katika nchi za Kiislamu wananyanyaswa kupita kiasi. Maisha yao hayana uhuru wala amani kwa kuwa sheria za dini yao zinawakandamiza wao na kuwapendelea wanaume. Hata hivyo, baadhi yao wanatambua hali hiyo na wanapambana kujaribu kuibadilisha. Lakini, ni wazi pia kuwa mapambano yao hayo hayawezi kuwasaidia sana kwa kuwa huko ni sawa na kusema Quran ibadilishwe. Je, hilo linawezekana kwa nchi hizo? Maana tatizo si wanaume au serikali; tatizo ni maagizo ya Mungu wanayemwabudu.


Katika video hiyo hapo juu, tunamwona mwanamke mtangazaji wa kituo kimojawapo cha TV kule Saudi Arabia, akimhoji mwanamke mwingine, Bi. Buthayna Nasser, ambaye naye ni mtangazaji kwenye kituo cha TV. Mahojiano yanahusu mjadala uliokuwamo kati ya wanazuoni wa Saudia juu ya wanawake kuonyesha nyuso zao kwenye TV ya Saudia.