Friday, March 15, 2013

Majibu Yangu kwa Ibrabura - Sehemu ya 1




Katika makala haya, ninajibu hoja zako rafiki yangu Ibra, ambazo umezitoa kwenye sehemu ya ‘comments’ kwenye makala yangu mengine yenye jina:  Je, Yesu aliagiza wafuasi wake wawaue maadui wa Yesu? Unaweza kusoma HAPA.


Ninatoa majibu yangu kama makala tofauti kwa sababu kuu mbili. Kwanza ni kuwapa fursa watu wengine waweze kujifunza kutokana na mjadala wetu na hata kuchangia au kutusahihisha pale tunapokosea. Pili, kutokana na urefu wa majibu yangu, ni rahisi kuyatoa kama makala kuliko maoni (comments), maana maoni ya mara moja hayatakiwi kuzidi herufi takribani 4,000 hivi.