Tuesday, January 14, 2014

Eti Yesu Amelaaniwa Hawezi Kuokoa




Kwenye facebook kuna hoja nyingi zinazozungumziwa humo. Nikakutana na ndugu mmoja mwislamu anatoa hoja kwamba Yesu amelaaniwa, hivyo hana uwezo wa kuokoa mtu. Na anatoa kabisa maandiko ya Biblia, eti kuthibitisha hoja zake - si kwa kudhihaki, bali kwa kuamini kabisa kwamba hivyo ndivyo ilivyo! Na hivi ndivyo hali ilivyo kabisa kwa Waislamu linapokuja suala la kutafuta sababu za wao kuukataa wokovu wa Yesu Kristo.

Monday, January 6, 2014

Maswali yangu kwako Mwislamu




Tarehe 21 Desemba 2012 niliuliza maswali yafuatayo HAPA. Lakini umepita mwaka mzima bado sijapata jibu japo kwa swali hata mojawapo tu! Ina maana maswali haya hayana majibu kutoka kwenye Quran au labda ndugu zangu Waislamu hawajayaona? Of course mimi binafsi najua kuwa hawawezi kuyajibu kwa sababu Uislamu hauna majibu juu ya masuala ya rohoni.

Hata hivyo, ningependa niyaulize kwa mara nyingine tena hapa tunapoanza mwaka huu wa 2014 ili iwe changamoto kwa Mwislamu uwaye yote – ujihoji, ujiulize na ujipime kule uendako.