Sunday, February 10, 2013

Baada ya Kuijua Njia ya Kweli, Mwana wa Kiongozi wa Hamas Auacha Uislamu na Kumgeukia Yesu Kristo







Mosab Hassan Yousef ni kijana wa kipekee ambaye ana ushuhuda usio wa kawaida. Baba yake ni mmoja wa waliokuwa viongozi wenye ushawishi mkubwa sana ndani ya kundi la kijeshi la Hamas kule Ukanda wa Magharibi (Palestina). Mosab alikulia kwenye familia iliyoshikilia Uislamu kwa nguvu sana.

Akiwa na umri wa zaidi ya miaka 30 sasa [yaani wakati ushuhuda huu ukiandikwa], ni mshirika wa Kanisa la Kikristo, Barabbas Road kule San Diego, Calif. Aliikana imani yake ya Uislamu, akaiacha familia yake kule Ramallah na anatafuta hifadhi ya kisiasa kule Marekani.

Hadithi ya maisha yake inashangaza sana - uwe unakubaliana au hukubaliani na mtazamo wake. Video ifuatayo inaonyesha mahojiano kati ya Mossab na kituo cha FOX News, akieleza yeye mwenyewe namna Muislamu kutoka Ukanda wa Magharibi alivyogeuka na kuwa Mkristo wa Pwani ya Magharibi.