Thursday, January 17, 2013

Yesu Mwenyewe Asema na Mwanamke wa Kiislamu



Mungu alinijibu Mimi!

Huu ni ushuhuda wa kweli kuhusiana na maisha ya mtu aliyekuwa anamtafuta Mungu.

Habari yako na Mungu akubariki. Jina langu ni Amal na ninashuhudia kwamba kile ambacho unaenda kusoma ni cha kweli kabisa na sahihi kwa kadiri ya kumbukumbu zangu maana Mungu mwenyewe ni shahidi yangu. Maombi yangu ni kwamba Mungu aseme  na moyo wako na kutumia ushuhuda huu kukubariki wewe kwa namna ya pekee maishani mwako.

Kimsingi mimi nilikulia kwenye familia ya Uislamu mkali. Baba yangu ni Mpalestina kutoka Israeli. Mama yangu ana asili ya Brazili. Alikuwa ni Mkatoliki. Baba yangu alikutana naye Brazili. Walioana na mama yangu alibadili dini na kuwa Mwislamu.

Tuesday, January 15, 2013

Hata Saudi Arabia Bwana Yesu Ameingia


Mhalifu wa kidini akihukumiwa kwa mujibu wa sharia
[Kama unachofanya ni kizuri; ni cha Mungu, kwa nini ufiche uso?]

Waislamu Wanazidi kukutana na Yesu

na Grantley Morris
‘. . . shuhuda zaidi na zaidi zinakuja kutoka kwenye nchi zilizofungwa juu ya Mungu anavyowapa Injili Waislamu kwa namna isiyo ya kawaida kupitia ndoto na maono. Miongoni mwa maelfu ya waamini katika Irani katika miaka michache iliyoisha, zaidi ya nusu yao wamekuwa waamini baada ya Yesu mwenyewe kuwatokea katika ndoto au maono.’ Wendell Evans wa the Billy Graham Center’s Institute for Muslim Studies anazungumzia juu ya wingi wa ndoto na maono yanayoripotiwa kuhusu Kristo miongoni mwa Waislamu . . .’

Kuzimu

Abdullah alikuwa Mwislamu mwaminifu. Aliishi umbali wa kama saa moja hivi kwa mwendo wa gari kutoka Makka. Alikuwa akiswali mara tano kwa siku, na mara kwa mara alitembelea Makka.

Kama ilivyo kwa Waislamu wengi, Abdullah alifundishwa kuwa Wakristo wana pepo wachafu na kwamba anatakiwa kujiepusha nao.

Usiku mmoja Abdullah aliota ndoto kwamba yuko kuzimu, anaungua moto. Asubuhi iliyofuata, akiwa ana wasiwasi mkubwa, aliomba kwa Allah, ‘Nimefanya kila kitu vizuri; kwa nini niende motoni?’ katika ziku zilizofuata, aliendelea kupata wasiwasi zaidi.

Sunday, January 13, 2013

Jambo la Ajabu Linaendelea Kwenye Ulimwengu wa Kiislamu




Makala haya yanaelezea mahojiano yaliyofanywa na mtangazaji wa CBN, Chris Mitchel, kuhusiana na kile kinachoendelea katika ulimwengu wa Kiislamu, ambao kwa karne nyingi umekuwa ukipinga kabisa Injili kuhubiriwa kwenye sehemu hiyo. Mahojiano haya yanaonyesha jinsi ambavyo Bwana Yesu mwenyewe anabomoa kuta na vizuizi kwa namna ambayo hata tawala za kiimla zinazotumia mahakama, hukumu za kifo na sheria kali kuzuia Injili kuwafikia watu, hawana tena la kufanya. Ni wakati wa Waislamu kujihoji na kumpokea Mwokozi wao ambaye aliwafia msalabani.

Mwanamke Mwislamu Aliyemkimbilia Yesu Kristo


Hii si picha ya Siti mwenyewe. Ni picha tu kutoka kwenye mtandao.

Ushuhuda wa Siti Zainab

Assalam-mualaikum.

Jina langu ni Siti Zainab. Mimi ni mwanamke wa Kiislamu kutoka Malesia, kusini mashariki mwa Asia.  Nilizaliwa kwenye familia ya Kiislamu, iliyokuwa ikifuata taratibu za Kiislamu kwa nguvu sana. Tokea mwanzo, nilipata elimu ya Kiislamu ambayo ilikuwa imara na ya ndani sana.

Pamoja na elimu yangu ya msingi, nilipelekwa pia kwenye madrasah ya Kiislamu, yaani shule ya dini, na nikaanza kusoma na kukariri Quran tangu mapema; huku nikijifunza maadili na misingi ya Uislamu wa Kisuni, kutoka kwa walimu waliobobea wa Kiislamu. Huko nilijifunza kumwogopa na kumtii Allah s.w.t. na pia kufuata mafundisho na mifano ya Mtume Muhammad (hususani yale yaliyo kwenye Hadithi zinazokubalika). Pia nilikuwa nina uwezo wa kusoma Quran yote, jambo ambalo liliwafurahisha wazazi wangu. Kwa kifupi, nilikuwa nina msingi imara na imani ya ndani ya dini kama Muslimah mwaminifu na aliyejitoa kwa moyo wote.

Saturday, January 12, 2013

Kwa Nini Niliacha Uislamu na Kumpokea Yesu?




Mutee'a Al-Fadi alikuwa ni Mwislamu mwenye msimamo mkali wa Wahabbi ambao alisomea kule Saudi Arabia. Lakini baada ya kukutana na upendo wa Yesu, moyo wake uligeuka kabisa na akaanza kuitafuta kweli iliko. Hatimaye alitambua kuwa Yesu ndiye Njia, Kweli na Uzima. Ufuatao ndio ushuhuda wake:

Friday, January 11, 2013

Je, Muhammad Ametabiriwa Kwenye Biblia? – Sehemu ya II




Katika makala yaliyopita tuliona hoja za ndugu wa Kiislamu wanavyojaribu kwa juhudi nyingi kuonyesha kwamba Muhammad ametabiriwa kwenye Biblia.

Katika makala hayo niliahidi kuwa nitaeleza jinsi ambavyo hoja zao hazina ukweli wowote. Licha ya kwamba Mungu wanayemwamini amewahakikishia kwamba Muhammad ametajwa kwenye Biblia, ukweli ni kwamba hajatajwa hata kidogo!

Monday, January 7, 2013

Je, Muhammad Ametabiriwa Kwenye Biblia? - Sehemu ya I



 Marehemu Ahmed Deedat

Waislamu wanashikilia kwamba Muhammad alitabiriwa kwenye Biblia. Andiko lao kuu wanalotumia kutetea hoja hii ni Kumbukumbu la Torati 18:18. Andiko hilo linasema:

Mimi nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


Haya ni maneno ambayo aliambiwa Musa na Yehova.


Mmojawapo wa watu ambao walijaribu sana kuonyesha kuwa andiko hili lilimhusu Muhammad, alikuwa ni mwanaharakati wa Kiislamu, marehemu Ahmed Deedat wa Afrika Kusini.