Monday, March 4, 2013

Je, Yesu Aliagiza Wafuasi Wake Wawaue Maadui wa Yesu?


Katika makala yangu niliyoipa kichwa kisemacho: Je, Muhammad Ametabiriwa Kwenye Biblia? – Sehemu ya II, yaliyo hapa; ambayo kimsingi ninaonyesha kimaandiko kwamba Muhammad kamwe hajatabiriwa kwenye Biblia, rafiki yangu Ibra kwenye sehemu ya maoni (comments) umenipa changamoto mojawapo ya muhimu sana.

Unasema: Mr. James, Kitu kibaya kwako ulichokiona kimeandikwa ndani ya qurani ni juu kuwachinja watu waovu? Sasa kama ndio hivyo, wewe hujasoma biblia au biblia hauijui vizuri. Unafanana na mtu wa kucopy na kupaste.