Sunday, March 17, 2013

Maswali Yanayonitatiza Kuhusiana na Quran



Ibra na Waislamu wengine, kumekuwa na kawaida kwa ulimwengu wa Kiislamu kufanya kila juhudi kuonyesha kwamba Biblia imepotoshwa, ingawaje jambo hilo si kweli hata kidogo. Ukiachilia mbali makosa ya kibinadamu ya hapa na pale ambayo yanaingia kutokana na ukweli kwamba Biblia imetafsiriwa na inaendelea kutafsiriwa mara nyingi sana, hakuna makosa ya makusudi yanayofanywa ili kupotosha au kuficha ukweli.

Na juhudi hizi zote zinafanywa ili kutaka kuonyesha kwamba  Quran ni neno la Mungu la kweli ambalo halijapotoshwa hata kidogo. Basi mimi naomba mnisaidie majibu ya maswali haya machache kati ya mengi:

Majibu Yangu kwa Ibrabura - Sehemu ya 2



JE, BIBLIA NI KITABU KILICHOPOTOSHWA?

Yeremia 8:8 inasema kwamba: Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.


Waislamu walipoona maneno haya: “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo,” kama kawaida, wakajua kuwa huu tayari ni ushahidi kwamba Biblia imetiwa maneno ya uongo, kwa hiyo si Neno la Mungu na haiwezi kuaminika.


Lakini mara zote ni lazima kwenda kwenye muktadha wa kila andiko au hoja ili kuona kama kweli hoja hizo zina nguvu ya kusimama.

Biblia na Quran ni Vitabu Vyenye Nguvu Sana



Historia ni kama ghala kubwa ambamo kumehifadhiwa kila kitu. Tunapochungulia kwenye ghala hili, tunaweza kujifunza kuhusiana na wapi tumetokea, na hatimaye wapi tuliko na kule tunakoelekea.

Bila shaka Biblia na Quran ni vitabu viwili ambavyo vina umuhimu mkubwa sana kwa wanadamu na ulimwengu. Hivi ni vitabu ambavyo ndivyo vinavyoumba maisha halisi ya idadi kubwa sana ya watu. Haya si tu maisha ya kula, kunywa na kuvaa hapa duniani, lakini pia vinaaminika kuwa vimebeba hatima ya milele yote kuhisiana na kila mwanadamu.