Saturday, July 6, 2013

Je, ni Kweli Quran Haijawahi Kubadilika na Wala Haina Mkono wa Mwanadamu Ndani Yake?




Utangulizi
Rafiki yangu Ibra, amekuwa akinishambulia sana kwa kusema kuwa Biblia ni kitabu kisichoaminika bali Quran ndiyo inayopaswa kuaminiwa. Hoja yake kuu, kama ilivyo kwa Waislamu wengine wengi ni kwamba, Biblia imeingizwa maneno ya kibinadamu kiasi kwamba yale ambayo Mungu aliyateremsha ni kama hayapo tena leo.

Katika makala haya ninapenda tuangalie swali kwamba: Je, ni kweli Quran ni kitabu ambacho hakijawahi kubadilika? Je, ujumbe wake ndio uleule ambao aliteremshiwa Muhammad na Allah? Je, ni kitabu cha kuaminika kuliko Biblia kama wanavyosema Waislamu?