Tuesday, January 15, 2013

Hata Saudi Arabia Bwana Yesu Ameingia


Mhalifu wa kidini akihukumiwa kwa mujibu wa sharia
[Kama unachofanya ni kizuri; ni cha Mungu, kwa nini ufiche uso?]

Waislamu Wanazidi kukutana na Yesu

na Grantley Morris
‘. . . shuhuda zaidi na zaidi zinakuja kutoka kwenye nchi zilizofungwa juu ya Mungu anavyowapa Injili Waislamu kwa namna isiyo ya kawaida kupitia ndoto na maono. Miongoni mwa maelfu ya waamini katika Irani katika miaka michache iliyoisha, zaidi ya nusu yao wamekuwa waamini baada ya Yesu mwenyewe kuwatokea katika ndoto au maono.’ Wendell Evans wa the Billy Graham Center’s Institute for Muslim Studies anazungumzia juu ya wingi wa ndoto na maono yanayoripotiwa kuhusu Kristo miongoni mwa Waislamu . . .’

Kuzimu

Abdullah alikuwa Mwislamu mwaminifu. Aliishi umbali wa kama saa moja hivi kwa mwendo wa gari kutoka Makka. Alikuwa akiswali mara tano kwa siku, na mara kwa mara alitembelea Makka.

Kama ilivyo kwa Waislamu wengi, Abdullah alifundishwa kuwa Wakristo wana pepo wachafu na kwamba anatakiwa kujiepusha nao.

Usiku mmoja Abdullah aliota ndoto kwamba yuko kuzimu, anaungua moto. Asubuhi iliyofuata, akiwa ana wasiwasi mkubwa, aliomba kwa Allah, ‘Nimefanya kila kitu vizuri; kwa nini niende motoni?’ katika ziku zilizofuata, aliendelea kupata wasiwasi zaidi.

Siku moja alishindwa kulala kabisa kwa sababu ya hofu. Usiku ule kulitokea mwanga mkali ulioangaza chumba chake na akasikia sauti inasema, ‘Mimi ni Yesu. Njoo kwangu. Mimi ni njia ya kwenda mbinguni. Nifuate mimi nawe utaokolewa na ule moto.’ Abdullah alianguka chini huku akilia na akasema, ‘Tafadhali, nisaidie namna ya kukupata.’

Baada ya siku chache Abdullah alipata Biblia na akaanza kuisoma. Baada ya muda mfupi aliyatoa maisha yake kwa Yesu. Akiwa sasa amejawa na furaha, alianza kuwaeleza familia na marafiki zake kuhusu imani yake mpya. Hata hivyo, kulingana na  sheria za nchi yake, Mwislamu anayeacha imani yake ni lazima auawe. Familia ya Abdullah walimkabidhi kwa mamlaka. Matokeo yake aliwekwa gerezani na kuteswa kwa miezi mingi.

Abdullah alipokataa kumkana Yesu, alipelekwa kwenye mahakama ya sharia, mahali ambako wahalifu wakubwa kabisa huhukumiwa. Jaji alimwambia Abdullah, ‘Kana hiyo imani yako mpya nawe utaachiwa huru kabisa. Kama ukikataa, utakatwa kichwa.’

“Sitamkana Yesu kamwe,” Abdullah alijibu, “Kama mkiniua nitaenda mbinguni. Lakini damu yangu itakuwa kwenye mikono yenu.” Abdullah alihukumiwa kukatwa kichwa Ijumaa iliyofuata.

Wakati akingoja siku hiyo ifike, Abdullah alirudishwa gerezani na akafungwa mikono na miguu. Siku ya kuuawa, hata hivyo, hakuna mtu aliyetokea! Jumatatu asubuhi iliyofuata walinzi walikuja wakamfungua minyororo yake na kusema, “Kimbia ewe pepo. Hatutaki kukuona tena!”

Akiwa haamini masikio yake, Abdullah aliomba kuelezwa ni kwa nini imekuwa hivyo. Walinzi wakamwambia kwamba katika siku ambayo alitakiwa kuuawa, mtoto wa jaji alikufa ghafla. Matokeo yake jaji alibadilisha ile hukumu.

Kama ilivyo kwa Wasaudia wengi, Abdullah alitoka kwenye familia ya kitajiri na alikuwa na kila kitu alichohitaji. Lakini matokeo yake, si tu kwamba alikataliwa na familia yake, bali sasa alikuwa hana tena kipato. Na alikuwa hawezi kupata kazi maana alihesabiwa kuwa msaliti. Vyeti vyake  vyote alinyang’anywa na angeweza kukamatwa tena wakati wowote.

Lakini licha ya ugumu wote huo,  Abdullah aliendelea kuishi Saudi Arabia kwa miaka kadhaa huku aliwahubiriwa wengine habari za Yesu.

*******************

Ndugu msomaji, Bwana Yesu yuko kazini Yeye mwenyewe. Sheria kali za kuwanyima watu uhuru wa kuamua juu ya hatima zao hazitafanikiwa kuzuia ujumbe wa uzima kuwafikia. Mwanadamu hawezi kamwe kushindana na Muumba wake. Fungua tu macho na masikio yako. Utashuhudia mengi. Lakini cha muhimu zaidi, mpokee Yesu awe Bwana na Mwokozi wako sasa.

Ushuhuda huu unapatikana kwa lugha ya Kiingereza hapa.

Waweza kuniandikia maoni yako pia kupitia: ijuekweli77@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment