Sunday, April 21, 2013

Mamilioni ya Waislamu Afrika Wanamkimbilia Yesu Kristo Isivyo Kawaida





 “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika 
ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa 
yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja” 
(Mathayo 24:14).

Ukisoma kurasa mbalimbali za kwenye mtandao juu ya kukua kwa dini ya Kiislamu, utakuta wengi wanasema kwamba Uislamu ni dini inayokua kwa kasi sana. Je, hilo ni kweli? Ni jambo gani linaloonyesha ukweli wa hoja hiyo?

Lakini tunao ushahidi wa Neno la Kristo kwamba siku za mwisho (yaani hizi tulizo nao), Injili itahubiriwa ulimwenguni kote. Pia, Mungu Yehova anaahidi kuwa hizi ni siku za kumwaga Roho wake kwa wanadamu wote. Hakika hizi ni nyakati za Injili ya Yesu Kristo kusonga mbele na kushinda na kubomoa kila upinzani na ukuta uliojengwa na adui ili kuwazuia wanadamu kumjua Mungu wa kweli na Mwokozi pekee, Yesu Kristo.

Uzuri ni kwamba, hili si jambo la mwanadamu. Hii ni kazi ya Mungu, Muumba mbingu na nchi Yeye mwenyewe. Ukristo si kama dini zingine ambazo zinajipigania zenyewe. Ukristo ni kazi ya Kristo mwenyewe! Kuipinga kazi hii ni kupingana naye. Na kuikataa kazi hii ni kumkataa Yeye mwenyewe. Mamilioni ya Waislamu wametambua sasa ni wapi uzima uliko.

Je, ndugu msomaji, umeshaingia kwenye safina ambayo ni Yesu Kristo? Usikubali kuachwa nje ya safina. Hakuna wokovu kwa mwingine awaye yote ila kwa Yesu Kristo peke yake!

Suala si dini. Suala ni maisha ya amani na furaha na mafanikio hapa duniani na kisha uzima wa milele mbinguni baada ya maisha haya. Dini hazitusaidii lolote kamwe – iwe ni Ukristo au dini nyingine!

Kama ingekuwa ni kuhesabu mafanikio ya dini katika historia nzima ya mwanadamu, basi dini zimefanikiwa sana kuleta mafarakano, chuki na uhasama baina ya wanadamu. Hakika hicho ndicho ambacho dini zimefanikiwa kufanya! Lakini Yesu – ah Yesu! Bwana wa amani! Bwana wa upendo! Bwana wa uzima na uzima tele! Yeye ni njia, ni kweli, ni uzima! Dini bila Yesu ni kupoteza kila kitu …!

Yafuatayo ni mahojiano kati ya mtangazaji Maher Abdallah wa kituo cha Al-Jazeera na Sheikh Ahmad Al Katani kuhusiana na suala la Waislamu milioni 6 kuingia kwenye Ukristo kila mwaka.

****************

Mtangazaji Maher:
Idadi ya Waislamu hivi sasa haizidi theluthi ya watu wa bara lote la Afrika.  Hii inatilia maanani pia ukweli kwamba, sehemu kubwa ya Waislamu katika Afrika ni Waislamu wa Kiarabu. (Yaani ambao wanapatikana kaskazini mwa Afrika).

Ni wazi kuwa suala la uinjilisti na kuwageuza watu kuwa Wakristo kunakofanywa na Wakristo vimesaidia katika kugeuza hali hii ya mambo katika bara hili.

Katika kujadili mada hii, ninayo furaha kumkaribisha mtu ambaye ni mtaalamu wa suala hili la uinjilisti na kuwageuza watu kuwa Wakristo katika Afrika. Atalenga kwanza kuzungumzia zaidi suala la kuenea kwa Ukristo. Shekhe Ahmad Al Katani, rais wa Companions Lighthouse for Science in Libya, ambayo ni taasisi iliyojikita kwenye kusomesha maimamu na wahubiri wa Kiislamu.

Shekhe Ahmad:
Katika hali halisi, maneno haya (yaani ya Maher) hayasemi kikamilifu kile kinachotakiwa kusemwa. Kama tulivyosema mwanzoni, kila mtu anayo haki ya kuwakaribisha wengine kwenye dini yake; hiki ndicho kinachojulikana kama kuhubiri dini. Na kuhusu uenezaji wa Ukristo, hakuna mtu mwenye haki ya kuwatoa Waislamu nje ya dini yao, na umeuliza kuhusu rejea na rejea ziko nyingi sana.

Uislamu ulikuwa ni dini kuu ya Afrika na kulikuwa na lugha 30 za Kiafrika ambazo zilikuwa zikiandikwa kwa maandishi ya Kiarabu. Idadi ya Waislamu imepungua Afrika hadi milioni 316, ambapo nusu ya hao ni Waarabu wa Afrika Kaskazini. Kwa hiyo, katika eneo la Afrika ambalo tunalizungumzia, eneo lisilo la Waarabu, idadi ya Waislamu haizidi watu milioni 150. Tunapotambua kwamba Afrika ina watu bilioni moja, tunaona kwamba idadi ya Waislamu imepungua sana kutoka idadi iliyokuwapo mwanzoni mwa karne iliyopita.

Kwa upande mwingine, idadi ya Wakristo imeongezeka kutoka milioni moja mwaka 1902 hadi milioni 329, 882,000, au tuseme milioni 330 mwaka 2000.

Kila saa moja, Waislamu 667 wanaingia kwenye Ukristo. Kila siku moja, Waislamu 16,000 wanaingia kwenye Ukristo. Kila mwaka mmoja, Waislamu milioni 6 wanaingia kwenye Ukristo. Idadi hii ni kubwa sana.

Mwandishi Maher:
 Hebu subiri kidogo. Unamaanisha ni Waislamu milioni 6 wanaingia kwenye Ukristo au wanaingia kwenye dini zingine?

Shekhe Ahmad:
Dini zingine haziwekwi kwenye kundi la kufanywa Wakristo; bali zinawekwa kwenye kundi la uinjilishaji. Dini nyingine katika Afrika ni upagani. Kwa hiyo ni Uislamu, Ukristo au upagani. Hakuna kitu kama kule Asia, kwa mfano, ambako kuna Ubudha au Uzoroasta. Kwa Afrika ni makundi haya matatu tu. Kwa hiyo, unapozungumzia kuhusu kuwafanya watu kuwa Wakristo, kunalenga dini nyingine pekee ya mbinguni, ambayo ni Uislamu.

*******************

Nini maana ya hali hii?  
[Maelezo yangu mimi blogger]
 
Maandiko Matakatifu yako wazi kwamba: wa kwanza atakuwa wa mwisho (Mathayo 19:30).  Ulaya na Marekani zilianza kuupokea Ukristo na kiwango kikubwa sana. Lakini hivi sasa wamemkataa Bwana Yesu na wanazidi kuzama zaidi na zaidi kwenye giza nene.

Afrika, ambayo ilikuwa katika giza nene la ibilisi la kutomjua Bwana huko nyuma, (kwa maana kwamba ilikuwa ya mwisho), katika nyakati hizi za mwisho, ndiyo inayokuwa ya kwanza. Nuru ya Injili inasambaa kama moto wa nyika. Na hili ni jambo linalotoka kwenye kiti cha enzi cha mbinguni kwenyewe kama nilivyosema hapo mwanzo.

Hata kama adui atajaribu kujiinua kwa kiasi gani, Neno la Bwana, kama kawaida yake, ni lazima litimie! Hata nukta moja haitaanguka hadi yote yatimie.

Ndugu msomaji, hebu jiulize mwenyewe, Ukristo haujawahi kushindana na mwanadamu ili kuwaingiza wanadamu kwa nguvu ndani yake. Haujawahi kushika panga wala bunduki ili kuwaingiza wanadamu kwenye imani hii! Sasa ni kitu gani kinachoufanya ukue kwa kasi namna hii? Mbona imani ya Kikristo ni imani ya upole, huruma, msamaha na maelewano lakini wakati huohuo inasonga mbele kwa kasi namna hii?

Bila shaka iko nguvu nyingine iliyo nyuma ya kundi hili. Nguvu hiyo ni Roho Mtakatifu, ambaye ni Mungu mwenyewe. Vita ya kanisa la Kristo siku zote imekuwa dhidi ya ulimwengu wa giza wa ibilisi. Na kwa sababu silaha zetu ni za kiroho (si za kimwili), hizo ni silaha za ushindi daima. Kanisa kamwe halishindani na wanadamu.

Bwana anatupenda sana wanadamu wake aliotuumba, ndiyo maana alikuja duniani na kuishi na kufa kwa ajili yetu. Mtu yeyote anayeshindana na Bwana hawezi kufika kokote. Tena ukichukulia kwamba mtu mwenyewe anashindana kwa silaha za kimwili dhidi ya silaha za kiroho!

Tafakari.

Jiulize.

Hoji mambo.

Chukua hatua.

4 comments:

  1. Huu ni uongo wa dhahiri ili kuupigia debe ukiristo.Iwapo watu 667 wanaingia kwa ukiristo kwa saa,na 327 milioni kwa mwaka,sidhani kama kungekuwa na Uislamu duniani kwa sasa.You are saying the direct opposite of that.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kama huu ni uongo, basi hilo ni jambo la ajabu kuliko kawaida. Shekhe Ahmad ni mwislamu, anaishi kwenye nchi ya kiislamu, na anaamini kuwa uislamu ndiyo njia ya kufika mbinguni. Huyuhuyu ndiye anayesema maneno haya, si kwa kukisia, lakini kutokana na utafiti waliofanya kitaalamu.

      Vinginevyo ndugu, labda unataka kutuambia kuwa huyu anayesema hivi ni mkristo ambaye amejipachika jina la kiislamu ili kuuchafua uislamu, au siyo?

      Lakini kama ni mwislamu, anapata faida gani au uislamu unapata faida gani kwa maneno yake haya kama si watu kuukimbia zaidi?

      Nilidhani yeye kama mwislamu, alitakiwa aseme kinyume chake kwa ajili ya kulinda heshima na jina la uislamu.

      Mimi nikiwa kinyume nawe, halafu ikatokea nataka kusema uongo juu yako, siwezi kusema uongo ambao utakujenga; nitasema uongo unaokubomoa!

      Delete
  2. Mie Regy....Mungu akubariki James kwa nguvu ulizonazo za kuutetea ukweli siku zote, ninachotaka kusema ni hiki yumkini alikosea tuu hesabu kwani sie si binadamu? maana nimesoma mada hapo juu inajieleza vizuri sana tuu cha msingi tuwe waelewa na kuwaombea Mungu wasio mjua Yesu wabadilike ishu sio kumpinga mwingine na kumwita mwongo,, haya kaandika amepata faida gani? maana sidhani kama James kamlipa kwa uongo wake............tuwe watu wenye akili jamani sii kukurupuka tuu nakutamka maneno yasiyo na kibali mbele za Mungu. unajua Imani ni kitu Kidogo sana watu wengi wanadharau lakini ni jambo kubwa sana ukiamini maana kama Bikira Mariam kama hakumuamini yule malaika basi leo asingekuwa mama wa Yesu na kupata heshma kubwa yakumbeba mfalme.....angalia hata parapanda isije ikapigwa ukaambiwa ukakataa ukadhani ni mabomu ya mbagala. Mimi nakushauri ndg msomaji usiwe mwepesi wa hasira, kinywa chako kikatawaliwa na chachu ya ibilisi ukajikuta unapata gharama yakutengeneza na Mungu. Mungu akubariki kama umenielewa.

    ReplyDelete