Sunday, June 2, 2013

Akef Tayem, Mwislamu Kutoka Palestina Akutana na Bwana Yesu na Kuokoka - Sehemu ya 1





Yafuatayo ni mahojiano kati ya mtangazaji, Sid Roth na Akef Tayem. Akef Tayem anatokea Palestina. Alikuwa ni Mwislamu lakini sasa anamwamini Yesu kama Bwana na Mwokozi wake. Pia anawapenda sana Wayahudi ambao zamani aliwachukia kwa moyo wake wote. Je, nini kilitokea? Hakika Bwana Yesu anahusika humo! Karibu ukutane na Bwana wa mabwana anayeweza kubadilisha maisha yako kwa namna ya kushangaza.

……………

Sid Roth:
Akef, hebu nieleze mtazamo wako ulivyokuwa kuhusiana na Wayahudi wakati wa ujana wako.

Akef:
Nilikua huku nikiwa nawachukia Wayahudi, maana walichukua ardhi yetu na kutuondoa kwenye makazi yetu.  Baba yangu alikuwa amefanikiwa sana kule Haifa, Israeli.  Lakini alishindwa sasa hata kuihudumia familia yake. Hivyo, niliwachukia Wayahudi.

Sid Roth:
Familia yako ilihamia Cyprus na kuanza upya. Lakini familia yenu ilikuwa ya watu imara sana, maana watoto wote waliweza kwenda kusoma Marekani. Na ulipokuwa Marekani, ulikutana na msichana mzuri wa Kikristo pale na akakueleza kuhusu Yesu. Hilo ni sawa, lakini jambo lililokuwa linakusumbua ni masuala ya miujiza. Kwa nini miujiza?

Akef:
Ni kwa sababu suala lenyewe lilikuwa halileti mantiki. Nilikuwa nikisomea Hisabati na Kemia; na unajua kwenye Uislamu, Muhammad hakuwahi kufanya miujiza yoyote. Kwa hiyo, kwetu miujiza si jambo lenye nguvu sana.

Sid Roth:
Msichana yule alikukaribisha kwenye mkutano wa injili. Kwa nini ulienda?

Akef:
Nilienda kwa sababu niliamini kuwa huyo mhusika alikuwa ni mhubiri wa uongo tu. Kimsingi nilikuwa siamini kuwa miujiza hutokea.

Sid Roth:
Ulipofika pale, uliona nini? Uliwaza nini?

Akef:
Kilichovuta hisia zangu, ilikuwa zaidi ni kama shoo – kuna magitaa pale, steji na watu wanamsifu Bwana …

Sid Roth:
Kwani hawafanyi hivyo msikitini?

Akef:
Hapana. Hapana. Kwenye Uislamu zaidi ni kuonyesha heshima, tunasujudu. Kwangu lilikuwa ni jambo geni kabisa. Lakini alipoanza kuongea kuhusiana na miujiza, kulikuwa na mtu kwenye kiti cha magurudumu, na mhubiri akasema angemwombea na angesimama.

Sid Roth:
Kwa hiyo alimwombea na akasimama?

Akef:
Ndiyo.

Sid Roth:
Kwa hiyo ulishuhudia muujiza?

Akef:
Sijui!

Sid Roth:
Unamaanisha nini unaposema hujui?

Akef:
Nilijua hiyo ni sehemu ya ile shoo. Kisha alimwita mwanamke aliyekuwa kipofu, akamwombea. Na mara akawa anaona. Kila kitu kilionekana kama kimepangwa tu. Kimsingi mambo hayo hayakunigusa hata kidogo. Kilichokuja kugusa moyo wangu, ilikuwa ni mtoto wa miaka kama 7 hivi. Na mtoto huyu hakuwa mbali na nilikokaa. Na mguu wake mmoja ulikuwa mfupi kuliko mwingine. Niliushuhudia maana walimpitisha karibu na nilikokaa. Mguu ulikuwa umepinda na ni mfupi.
Na yule mhubiri alisema kuwa wampeleke kwenye jukwaa; na kwamba angemwombea; na kwamba Mungu angemponya. Na cha ajabu, mhubiri huyo alisema, “Wale ambao hamuamini kuhusu miujiza, njooni huku mtaona jambo.” Nikaona kuwa hiyo ilikuwa ni fursa yangu. Niliruka na kwenda kwenye jukwaa.

Sid Roth:
Ukaona nini sasa?

Akef:
Alimkalisha mtoto yule mbele yake kwenye kiti mbele yangu. Kisha alishika mguu wa mtoto kwenye mikono yake. Na mimi nilisimama kwa pembeni ili niweze kuona vizuri. Alipoanza kuomba, ‘Katika jina la Yesu,’  ule mguu ulianza kurefuka hadi ukafikia urefu wa mguu mwingine, kisha ukakomea hapo. Na mwazoni mwangu nilikuwa nimewaza labda ungepitiliza. Jambo hilo sikuwa na uwezo wa kulikana! Kisha ukawa kama umejazwa hewa ‘puu’.

Sid Roth:
Uliona haya kwa macho yako mwenyewe?

Akef:
Niliona kwa macho yangu kabisa! Na cha kushangaza, mtoto yule alisimama na hakuweza kuukanyagia mguu ule sawasawa. Ilikuwa na kama amepata mguu mpya. Ilibidi ajifunze kuutumia. Ilimchukua dakika chache kung’amua kwamba kumbe anaweza kuukanyagia mguu ule. Na hatimaye akaanza kukimbia. Hilo, sikuweza kulikana!

Sid Roth:
Sasa, ukawa muumini wa Yesu Kristo. Familia yako ilichukuliaje hilo?

Akef:
Oh, oh. Ilikuwa msukosuko. Walinikataa. Walimwambia kaka yangu ambaye tulikuwa wanafunzi sote kunishawishi niachane na Ukristo. Alijaribu mara kadhaa. Alisema, “Umefanya hili. Baba hajafurahia.” [Maana alikuwa akigharamia mahitaji yangu yote]. “Unatakiwa urudi kwenye imani yetu.” Lakini sikuweza kufanya hilo. Kwa hiyo walinikataa.

Sid Roth:
Je, walikutemea mate?

Akef:
Unajua, hiyo ndiyo mila yetu. Inabidi wakutemee mate. Hiyo ndiyo namna ya kukukataa.

Sid Roth:
Kwa hiyo, ulikuwa kwenye msukosuko mkubwa.

Akef:
Ndiyo.

Sid Roth:
Baba yake alimkataa. Akef hakuingia kwenye mfungo, lakini alikosa kabisa hamu ya kula. Alikaa zaidi ya siku 40 bila kula chakula zaidi tu ya kunywa maji. Kisha muujiza ulitokea kwake!!

……………………………

Ndugu msomaji, kuna mambo makubwa yaliyotokea kwa Akef baada ya kupita kwenye kipindi hicho cha kutokula kwa siku hizo zote. Je, ni mambo gani hayo?

Tafadhali fuatilia sehemu ya pili ya ushuhuda huu wenye nguvu. Bwana Yesu ni halisi kama ambavyo Biblia inasema. Bofya HAPA.

..........................
 

Tafakari

Jiulize

Hoji mambo

Chukua hatua.

..........................
Bonus reading: click HERE.

No comments:

Post a Comment