Friday, April 18, 2014

Eti Wakristo Hula Mkate Wenye Mavi (au Mashonde)





Waislamu wanaojaribu kuitoa makosa Biblia bado wanaendelea na mahangaiko yao ya kujaribu kuipa uhalali quran kupitia upotoshaji mkubwa wa Maandiko ya Biblia. Kama kwaida, hawana hoja mpya wala za kufikirisha, bali ‘wana-recycle’ maswali yaleyale toka januari hadi desemba. Haya ni maswali ambayo yalibuniwa na watu fulanifulani, basi na wao wanayabeba bila hata ya kuchuja na kujua endapo yana ukweli au la. Hata hivyo, kila jambo wanalolisema kinyume na Biblia ni UONGO mtupu SIKU ZOTE - NA USHAHIDI WA UONGO HUO TUNAO WAZIWAZI!

Katika kitabu cha Ezakieli imeandikwa:

…. Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya mashonde yatokayo katika mwanadamu. (Eze 4:12).
[Maana ya mashonde ni kinyesi]


Hebu soma hoja mojawapo juu ya andiko hili kutoka kwa mmoja wa hawa ndugu:
Wakristo hivi mnafaham yakuwa huo Mkate una mavi? Mavi jamani mavi, mnalishwa mavi eti ni mwili wa mungu,
Someni ndani ya Biblia imeandikwa mashonde, ila Maana yake haswa ni mavi ya mwanaadam, hili andiko
EZEKIELI 4:12
Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya mashonde yatokayo katika mwanadamu.
Mashonde maana yake ni mavi makavu, anaebisha afunguwe Biblia yake sehemu ya maneno magumu.
Nyie kulenitu ila fahamuni mnakula mavi.
Mwisho wa kunukuu.


Biblia inaongea vizuri sana juu ya watu hawa:

Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe. Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu. (Warumi 10:1-3)



Ni kweli kabisa juhudi wanayo sana, tena sana! Lakini hebu chukulia mfano huu. Kila asubuhi Bwana Juhudi huenda kutega upepo kwa kutumia tenga ili aweze kuupata. Na anafanya hivyo kwa miaka yake yote anayoishi hapa duniani. Lakini inafika siku ambayo amezeeka, hana nguvu na yuko tu kitandani. Je, atakapojiangalia na kujipima katika kazi ile aliyofanya kwa miaka yake yote, kutakuwa na nini cha kumsaidia?


Ndicho hasa wanachofanya hawa ndugu zangu Waislamu wanapojaribu “kutuhubiria” Biblia – Mungu ni shahidi yangu – wanatega tu upepo kwa matenga!


Na kinachonishangaza na kunisikitisha ni jinsi ambavyo huongea kwa ujasiri kana kwamba kile wanachokisema kina hata chembechembe za ukweli!!


Basi hebu tuone tenga lao limenasa nini kwenye Ezekieli 4:12. Tusome tena andiko hilo:

…. Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya mashonde yatokayo katika mwanadamu. (Eze 4:12).


Hapa Mungu alikuwa amekasirishwa na wana wa Israeli kwa sababu ya uasi na dhambi zao. Kwa hiyo akamwambia Yeremia:


Lakini wewe, mwanadamu, tazama, watakutia pingu, nao watakufunga kwazo, wala hutakwenda nje kati yao; nami nitaufanya ulimi wako ugandamane na kaakaa lako, hata utakuwa bubu, wala hutakuwa mwonyaji kwao; kwa kuwa wao ni nyumba yenye kuasi. (Eze 3:25-26) 


Kwa hiyo Mungu akapanga kuwaadhibu. Lakini akataka kuwapa onyo kwanza ili kama wana akili wageuke na kuacha njia zao mbaya. Na maonyo hayo aliyatoa kupitia Ezekieli – kwamba afanye mfano wa kile ambacho kitawakuta kama wataendelea kuasi.


Acha tusome kabisa maneno hayo kikamilifu:


(Eze 4:1)  Wewe nawe, mwanadamu, jipatie tofali uliweke mbele yako, kisha, chora juu yake mfano wa mji, yaani, Yerusalemu;


(Eze 4:2)  ukauhusuru, ukajenge ngome juu yake, na kufanya boma juu yake; ukaweke makambi juu yake, na kuweka magogo ya kuubomoa yauzunguke pande zote.


(Eze 4:3)  Kisha ukajipatie bamba la chuma, ukalisimamishe liwe ukuta wa chuma kati ya wewe na mji huo; ukaelekeze uso wako juu yake, nao utahusuriwa, nawe utauhusuru. Hili litakuwa ishara kwa nyumba ya Israeli.


(Eze 4:4)  Tena lala chini kwa ubavu wako wa kushoto, ukaweke huo uovu wa nyumba ya Israeli juu yake; kwa kadiri ya hesabu ya siku utakazolala juu yake, kwa kadiri hiyo utauchukua uovu wao.


(Eze 4:5)  Maana nimekuagizia miaka ya uovu wao iwe kwako hesabu ya siku, yaani, siku mia tatu na tisini; ndivyo utakavyouchukua uovu wa nyumba ya Israeli.


(Eze 4:6)  Tena utakapozitimiza hizo, utalala kwa ubavu wako wa kuume, nawe utauchukua uovu wa nyumba ya Yuda; siku arobaini, siku moja kwa mwaka mmoja, nimekuagizia.


(Eze 4:7)  Nawe utauelekeza uso wako, uelekee mazingiwa ya Yerusalemu, na mkono wako utakuwa haukuvikwa nguo, nawe utatoa unabii juu yake.


(Eze 4:8)  Na tazama, nitakutia pingu, wala hutageuka toka upande mmoja hata upande wa pili, hata utakapozitimiza siku za mazingiwa yako.


(Eze 4:9)  Pia ujipatie ngano, na shayiri, na kunde, na dengu, na mtama, na kusemethi, ukavitie vyote katika chombo kimoja, ukajifanyie mkate kwa vitu hivyo; kwa kadiri ya hesabu ya siku utakazolala ubavuni mwako; yaani, siku mia tatu na tisini utaula.


(Eze 4:10)  Na chakula chako utakachokula kitapimwa, shekeli ishirini kwa siku moja; utakila kwa wakati wake.

(Eze 4:11)  Nawe utakunywa maji kwa kuyapima, sehemu ya sita ya hini; utayanywa kwa wakati wake.


(Eze 4:12)  Nawe utakila kama mkate wa shayiri, nawe utakioka mbele ya macho yao juu ya mashonde yatokayo katika mwanadamu.


(Eze 4:13)  Bwana akasema, Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyokula chakula chao, hali kimetiwa unajisi, kati ya mataifa nitakakowafukuza.


(Eze 4:14)  Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, tazama, roho yangu haikutiwa unajisi; maana tangu ujana wangu hata sasa sijala nyamafu, wala iliyoraruliwa na hayawani; wala nyama ichukizayo haikuingia kinywani mwangu.


(Eze 4:15)  Ndipo akaniambia, Tazama, nimekupa mashonde ya ng'ombe badala ya mashonde ya mwanadamu, nawe utakipika chakula chako juu ya hayo.



Kwa sababu ya kukariri vitu bila kujibidisha kutafuta ukweli, wahubiri hawa wa injili ya Kiislamu inayotoka kwenye Biblia, wanadhani eti Ezekieli aliambiwa apike mkate kwa kuchanganya na mavi ya mwanadamu. Pole yao!!  


Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe. Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu. (Warumi 10:1-3)


Lakini Biblia inasemaje?


Nawe utakila kama mkate wa shayiri, NAWE UTAKIOKA mbele ya macho yao JUU YA MASHONDE YATOKAYO KATIKA MWANADAMU. (Eze 4:12) 


Sijui Kiswahili ni kigumu kwao? Hapa Ezekieli anaambiwa atumie mavi ya mwanadamu kama kuni za kuokea; siyo kwamba ayachanganye ndani ya mkate!!


Na kwa sababu lengo lilikuwa ni kuonyesha mfano wa yale yatakayowakuta watenda dhambi hao, Mungu akafafanua maana ya jambo hilo:


Bwana akasema, Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyokula chakula chao, hali kimetiwa unajisi, kati ya mataifa nitakakowafukuza. (Eze 4:13) 


Maana yake ni kuwa, wataondolewa kwenye nchi yao na kusukumwa kwenye mataifa yasiyomjua Mungu; mataifa ya kipagani yanayoabudu miungu mingine; na huko wataishia kunajisika, maana itawabidi wale chakula cha hayo mataifa.


Lakini kwa sababu Ezekieli naye alijisikia vibaya kwa jambo hilo, ndipo Mungu akapunguza ukali wa lile jambo:


Ndipo akaniambia, TAZAMA, NIMEKUPA MASHONDE YA NG'OMBE BADALA YA MASHONDE YA MWANADAMU, nawe utakipika chakula chako juu ya hayo. (Eze 4:15) 


Acheni kukariri ndugu zangu Waislamu!! Mnaelekea kuzimu!!


Nimalizie kwa kuubainisha uongo wa walimu hawa (wa uongo) kwa kutaja mambo manne muhimu:

Kwanza: Mashonde hayakutiwa ndani ya mkate bali yalitakiwa kutumika kama kuni za kuokea mkate.

Pili: Hili si agizo la Mungu kwa Wakristo juu ya namna ya kupika mikate yao.

Tatu: Mkate huu hauna uhusiano na ule unaotumiwa na ndugu zangu Wakatoliki kwenye meza ya Bwana.

Nne: Jambo hili lilifanywa kama adhabu kwa Israeli kutokana na dhambi – sasa je, mkate unaoliwa Kanisani huwa ni kwa ajili ya adhabu?

Enyi wahubiri wa injili wa Kiislamu, mnayemdanganya ni ninyi wenyewe wala hamuwadanganyi Wakristo, maana kile mnachohubiri wala hakimo ndani ya Biblia. In fact, HAMJAWAHI HATA SIKU MOJA KUSEMA NENO LA BIBLIA NA LIKAWA KWELI. YOTE HUWA NI UONGO NA UPOTOSHAJI.

MBINGU IPO MOJA TU! MUNGU YUPO MMOJA TU NA JINA LAKE MOJAWAPO NI “YESU”. NENO LA MUNGU LIKO KWENYE KITABU KIMOJA TU – NACHO NI BIBLIA!!

Mnajihangaisha bure kutega upepo kwa matenga!!

9 comments:

  1. Na c ajabu huyu mtu akawa ni kiongozi wa msikitin

    ReplyDelete
  2. Na c ajabu huyu mtu akawa ni kiongozi wa msikitin

    ReplyDelete
  3. tatizo wao wanasoma ili wapinge bila hata upembuzi yakinifu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Uzuri ni kwamba Neno la Kristo ni upanga. Linakaa ndani yao na litawasumbua hadi wale waliokusudiwa watakapofunguka. Kazi yetu ni kupanda mbegu na kumwagilia. Bwana ndiye anayeotesha na kukuza.

      Delete
  4. Yesu yeye alikula mavi ya ng'ombe sio ya binadamu? Dah! huyo Mungu ana roho gani? Hana huruma wala haki? Hivi kwani Mungu wenu ni yupi na anasifa zipi? Maana mpaka sasa sijaona mkristo mwenye kumjua Mungu. Wengine wanasema Yesu Mungu. siwaelewi. Lakini nadhani tatizo kubwa ni biblia na mapokeo ndio tatizo. Wakristo wote wanamfuata mafundisho ya paul.

    ReplyDelete
    Replies
    1. shalom ndugu. asante kwa kutembelea blog hii na kutoa maoni yako - MAANA HYA NI MAONI KWELIKWELI. Post hii imeongea kwa ushahidi wa maandiko lakini wewe ulichotoa ni maoni tu ambayo hayana ushahidi wa hata andiko moja. Ni nani basi atakayeacha kufuata maandiko afuate maneno ya mtu yasiyo na support ya maandiko.

      Tunaheshimu maoni yako lakini tunasikitika kwamba hayana uzito wowote wa kutiliwa maanani.

      Delete