Ndugu zetu Waislamu
wanasikitisha sana; tena sana!
Katika Sefania 3:9 imeandikwa:
Maana hapo ndipo nitakapowarudishia
mataifa LUGHA ILIYO SAFI, wapate kuliitia jina la Bwana, wamtumikie kwa nia
moja.
Ndugu zetu wanadai huo ni utabiri wa
lugha ya Kiarabu ambayo ndiyo inayotumiwa kwenye Uislamu. Duh!
Wakati nabii Sefania akiandika ujumbe
huu, Mungu (Yahweh) alikuwa ameghadhibikia sana mataifa mbalimbali kwa sababu
ya kupenda uovu badala ya kupenda haki inayotokana na kumtii Yeye.
Ndipo akasema:
Basi ningojeni, asema Bwana, hata siku
ile nitakapoondoka kuteka mateka; maana nimeazimia kuwakusanya mataifa, ili
nizikutanishe falme, nipate kuwamwagia ghadhabu yangu; naam, ukali wote wa
hasira yangu; kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa wivu wangu. Maana
HAPO NDIPO NITAKAPOWARUDISHIA MATAIFA LUGHA ILIYO SAFI, wapate kuliitia jina la
Bwana, wamtumikie kwa nia moja. (Sefania 3:8-9)
Hebu tujiulize tu
swali rahisi la kimantiki:
Kwa kuwa hapa Mungu
ana hasira kali dhidi ya TATIZO LA UOVU;
na kwa kuwa SULUHISHO lake ni kuleta
LUGHA SAFI itakayosababisha mataifa yote yamwabudu kwa nia moja iliyo safi;
na
kwa kuwa ninyi ndugu Waislamu mnadai lugha hiyo ni Kiarabu –
je, iwapo wewe
ndugu mwislamu una vijana au binti zako ambao wamezama kwenye dhambi, mfano
uzinzi, uuaji, dawa za kulevya, ujambazi, nk –
JE, UKIWAFUNZA KIARABU WATAPONA?
Je, LUGHA INAWEZA KUBADILI MIOYO?
Je, lugha inaweza kumfanya jambazi akawa mtu mwema?
Je, jela zinaweza
kukosa watu kwa iwapo utawafunza wafungwa wote Kiarabu kweli?
Mbona mnaangamizana
wenyewe ndugu zetu kwa kulishana uongo?
Yesu ni Jibu la
maisha.
Tafakari
Chukua hatua
No comments:
Post a Comment